TENGENEZA MAADUI WAKO MWENYEWE

Katika kipindi changu cha ukuaji hasa katika elimu, kumekuwa na tabia  ya kuishi na watu/ kuwachukulia watu kutokana na historia zao za nyuma; katika kipindi hiki hasa mwenendo na tabia za walimu.

Katika safari yangu ya elimu miaka fulani nilipata bahati ya kwenda kusoma katika shule moja huko kaskazini mwa nchi, na kama mwanafunzi mgeni katik
a shule ile nilipata historia ya vitu vingi vizuri na vibaya ikiwemo taarifa za wakufunzi, yaani waalimu wa shule ile. Moja kati ya taarifa za walimu ilikuwa ni hii “Ohooh yaani huyu mwalimu wa bweni ni mnoko vya hatari kaa nae mbali, unaweza ukaona kama anakuchekea kumbe ndo anakuchomea kule ofisini, kuwa makini” na wanafunzi walikuwa wakimuogopa.

Baada ya muda kidogo, tukawa na mahusiano mazuri tu na mwalimu mpaka nikawa naacha vitu vyungu kwake,  ikiwemo pesa begi languo zisizo za shule na simu, ambavyo vitu hivyo ni haramu mwanafunzi kuwa navyo shuleni. Na nikihitaji wakati wowote navipata hasa simu kwa aajili ya mawasiliano. Uhusiano ulikuwa mzuri tu, na kwakuwa anaduka mtaani nikuwa nachukua saa dukani kwake na kuja kuwauzia wanafunzi wenzangu pale shuleni. Na mpaka nimemaliza nakuondoka mahusianao yapo vizuri kwamaana tuliendelea kuwasiliana vizuri.

Katika uhalisia wa maisha sehemu yoyote ile utakapoenda kwa mara yakwanza ni lazima utakuwana na wenyeji watakao kupokea na kukupa maelezo na ABC za mazingira hayo. Watu wengi katika kukueleza watasema mambo mengi ikiwemo kipi ni kizuri chakufanya/kuchagua na kipi ni kubaya na hupaswi kufanya.

Kwa  kawaida mtu huyo takueleza hisia zake juu ya mambo au mtu fulani kutokana na mambo aliyoyapitia akiwa na mtu huyo. Kwa mfano shuleni “mwalimu fulani kuwa nae mbali maana ni mtata sana” au kazini utasikia “Kaa mbali na boss Kipara maana ni mnoko sana”. Sasa katika hali ya kawaida wewe baada ya kuyasikia hayo yote ni lazima utatengeneza hali ya ‘tension’ unapokuwa katika miingiliano na hawa watu, kwasababu tayari ulishapandikizwa chuki na ubaya wao.

Sasa kimsingi, ni kweli hawa watu wanamabaya yao lakini hawakukufanyia wewe na huwenda pia ni mabaya ya muda kitambo kilichopita, lakini usipokuwa makini unajikuta na wewe unawachukia na kuwaona sio sahihi katika maisha yako, na kuwafanya kuwa maadui zako. Sikiliza, kwa kufanya hivyo unajitengenezea mazingira magumu katika safari ya kufanikiwa kwako, hapo kazini, shuleni, na sehemu yoyote ambayo unapita.

Kuwa na maadui ni kawaida katika maisha ya mwanadamu kwani inakupa namna ya kutatua vikwazo katika safari ya kimaisha, lakini hakikisha ni adui uliomtengeneza wewe mwenyewe, yaani chanzo cha uadui baina ya wewe na mtu mwingine kiwe na mahusiano ya moja kwa moja kati yako na mtu huyo. Usikubali kutengenezewa maadui.

Sir, Seth

Sharing life experience, as others can learn from i.

Post a Comment

Please Select Embedded Mode To Show The Comment System.*

Previous Post Next Post

How do i meet HDI

Success from other people's opinions