JENGA MTANDAO WA WATU


Njia Ya Mafanikio Katika Ulimwengu wa Utandawazi

“Usichokuwa nacho jirani yako anacho fanya mawasiliano jibu lako lipo karibu yako tu. Tatizo ni wewe umejifungia(Do not be Self-container to your development)” Stephin Fuime

Muda mwingine sababu kuu ya kupitia hali ngumu ni wewe mwenyewe, kwasababu hutaki kuzungumza na watu. Ukweli ni kwamba huyo jamaa ambaye wewe unamchukulia poa ndie mwenye jibu la tatizo lako, pata muda wa kuwafahamu watu wanaokuzunguka; yaweza kuwa majirani zako pale nyumbani, rafiki yako kule kazini, au watu katika eneo lako la la mzunguzo wa kila siku: ni muhimu sana kuwajua watu.

Piga picha kwamba wewe ni fundi gereji na una mteja wako ambae mara nyingi huwa unamtengenezea gari lake, na mahusiano yenu yamebaki hapo tu, yaani unamjua kuwa ni mteja wako pale kazini kwako (gereji) tu; hukutaka kujua zaidi kuhusu mteja huyo. Na ukweli ni kwamba mteja wako ni wakili maarufu tu. Sasa siku moja katika pilika pilika zako ukatakiwa passport ya kusafiria na katika mchakato wa kuipata inakubidi uende kwa wakili ila kuapa kwa aajiri ya taarifa za wazazi wako (affidavit). Swala hili lingekuwa rahisi sana kama ungekuwa unajua mteja wako wa kila wakati kule kazini kuwa ni mwanasheria kwa maana ungemtafuta  tu maramoja nae angefanya jambo, kwasababu wewe ni mtu unaemfanyia vizuri akija kupata huduma ofisini kwako kule gereji.

Miaka Fulani nilikuwa naishi makao makuu ya nchi, nilikuwa nimepanga chumba katika nyumba moja kubwa iliokuwa na vyumba vingi, bahati nzuri kulikuwa na mfanyakazi mwenzangu nayeye alikuja kupanga pale pale nilipokuwa nikiishi, maana ilikuwa ni nyumba kumbwa tu yenye vyumba vingi vya kupanga. Basi siku moja nikiwa natoka kazini jamaa angu alikuwa nyumbani siku hiyo hakwenda kazini, nikakutana nae maeneo ya nyumbani nje pale, kwakuwa mimi nilikuwa nimechoka nikamwambia jamaa angu kuwa vipi umepika jamaa akasema ana mawili apike au asipike maana alikuwa ameshiba sana, basi mimi nkamwambia hakuna tatizo, basi mimi nikiwa na uchovu wa kazi kutwa nzima niliingia ndani kwangu na kupika wali, wali ulivyokuwa tayari  kabla sijapika mboga nikapakuwa kidogo nikala kwa kuwa nilikuwa na njaa sana, mara nikaongeza tena na kujikuta nimeshiba tayari, hatimae nikajisemea mboga za nini tena natayari nishashiba, nikaendelea na mambo mengine: ilikuwa ni mida ya saa 12 jioni.

Baadae kidogo mida ya saa 3 usiku nikasema niende kumcheki jamaa ndani kwake, ghafla nikamkuta jamaa hana chakula anakula mboga; yaani ana mboga hana chakula, na mimi kule nilikula chakula bila mboga. Nikamwambia vipi kaka mbona unakula mboga tupu, njoo uchukue chakula nimepika acha ujinga, kwakuwa nilimuuliza kuwa kama atapika akasema hatapika, aliona haya na kusema “aah hamna shida bana usijali”.

Kisingi jamaa hakuwa na haja ya kulala na njaa kwa kula mboga pekee na mimi sikuwa na haja ya kula chakula bila mboga, pale nilipomuuliza kuwa “utapika  leo” angesema tuu kuwa mimi sina mpango wa kupika ila ninamboga tayari ndani kama wewe utaweza pika chakula mboga zipo, nakila mmoja wetu angekuwa mshindi

Katika ulimwengu huu wa utandawazi usujaribu kufungia mawazo yako kwenye boksi kubwa la ubinafsi, ongea na watu kwa sababu wataalamu wanasema, Ukitaka kufika nenda mwenyewe ila ukitaka kufika mbali nenda na wenzako. Hii inamaanisha umoja unanguvu zaidi kuliko kuwa pekeako katika kila jambo.

Wewe kijana niwakati wako wa kutengeneza mtandao wa watu sasa, ukisoma kitabu kinachoitwa His excellence the Head of State kinasema “The matter is not what you know but who you know” sasa kauli hiyo ikupe changamoto wewe, kwamba usiishie kujenga ujuzi tu, kwasababu ujuzi pekee hautoshi; unahitaji kuwajua watu katika eneo lako la ujuzi.

Sir, Seth

Sharing life experience, as others can learn from i.

Post a Comment

Please Select Embedded Mode To Show The Comment System.*

Previous Post Next Post

How do i meet HDI

Success from other people's opinions